• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Government Web Framework
Government Web Framework

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mwongozo wa Tovuti za Serikali

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Usafi na Manzingira
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na uhusiano
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki na Misitu
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Mipango
      • Kamati ya Masuala ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Elimu , Afya na Maji
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
    • Madiwani wa Kuchaguliwa
    • Madiwani wa Kuteuliwa
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Majarida
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Kanzi Data ya Picha
    • Hotuba
    • Habari
    • Video

TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA HALI YA LISHE WILAYA YA SHINYANGA KWA KIPINDI CHA NUSU MWAKA JULAI /DISEMBA 2023

Posted on: March 3rd, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Johari Samizi amewataka Watendaji Kata na Maafisa Elimu wa Halmashauri mbili za Wilaya ya Shinyanga kusimamia utekelezaji wa mpango wa chakula mashuleni ili kukuza kiwango cha ufaulu. Hayo ameysema wakati wa kikao cha Tathmini ya Mkataba wa Lishe kwa kipindi cha nusu mwaka Julai hadi Disemba, 2023  kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Manispaa ya Shinyanga Machi 01, 2024. Kikao hicho kimejumuisha watalaam kutoka ofisi ya Manispaa ya Shinyanga na Halmashauri ya Wilaya aya Shinyanga.


“ Kuna mahusiano ya moja kwa moja kati ya chakula na ufaulu wa masomo kwa watoto.Tafiti zinaonyesha watoto wanaopata chakula mashuleni wanafanya vizuri katika masomo, shirikisheni  wazazi na  tuendelee kutoa elimu kwa wazazi  hao kuhusu umuhimu wa watoto kupata chakula mashuleni...” alisisitiza Mhe. Samizi.


Akitoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za lishe katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Afisa Lishe wa halmasahuri hiyo, Bw. Said Mankligo amesema kuwa katika kipindi  cha nusu  mwaka Julai hadi Disemba, 2023, halmashauri imefanya shughuli za usimamizi  na utekelezaji wa mkataba wa Lishe . Shughuli hizo ni pamoja na utoaji wa nyongeza ya matone ya Vitamin A, dawa za minyoo na upimaji wa lishe kwa watoto chini ya miaka 5 uliofanyika katika kampeni ya mwezi Disemba 2023 kwa watoto 67,959 kati ya watoto waliotegemewa 67,951 sawa na 100.01%.


Shughuli zingine ni  utoaji wa vidonge vya kuongeza wingi wa damu (FEFO) kwa wajawazito wanahudhuria kliniki  katika vituo vya kutolea huduma za afya, upimaji wa hali ya lishe na matibabu ya utapiamlo mkali, utoaji wa elimu  ya unyonyeshaji na unasihi wa ulishaji sahihi wa chakula cha nyongeza kwa watoto.


Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Shinyanga amewataka Watendaji wa Kata kuhakikisha kuwa wanasimamia uanzishaji vitalu vya viazi lishe katika maeneo ya shule na kusimamia maelekezo yote yaliyotolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Lishe ya Wilaya ambaye ni Mkuu wa Wilaya hiyo ili kuwezesha mafanikio katika mpango wa Taifa wa masuala ya Lishe.


Mpango wa upatikanaji wa chakula mashuleni ni mojawapo ya afua inayolenga kuongeza afya za wanafunzi na kupunguza utoro mashuleni ikiwa ni Utekelezaji wa Mpango Jumuishi wa Kitaifa wa Masuala ya Lishe “National Multasectoral Nutrition Action Plan” (NMNAP) ambao ni  sehemu ya utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Lishe na Mkakati wa  miaka kumi (2015/16 – 2025/26). Mpango huo umeainisha afua mbalimbali za lishe zinazopaswa kutekelezwa nchini kwa lengo la kupambana na utapiamlo katika aina zake zote.


Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Johari Samizi akifungu kikao cha Tathmini 

ya Mkataba wa Lishe kwa kipindi cha nusu mwaka Julai hadi Disemba, 2023 

kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Manispaa ya Shinyanga Machi 01, 2024

Baadhi ya wajumbe wa kamati ya Lishe wakifuatilia kwa makini wakati wa kikao hicho


Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya Shinyanga, Bw. Said Mankligo akiwasilisha 

 taarifa ya utekelezaji wa shughuli za lishe katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga 

kwa kipindi cha nusu mwaka Julai hadi Disemba, 2023  


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 09, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA ( MCHUJO) KADA YA DEREVA DARAJA LA II April 15, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA TATU April 17, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI April 19, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MITI 1000 YAPANDWA KATA YA SALAWE KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 63 YA UHURU.

    December 09, 2024
  • BABA BORA, SAUTI YA UMMA NA WANAWAKE VIONGOZI WAPATIWA VITENDEA KAZI

    November 15, 2024
  • WANADIDIA WAOMBWA KUJITOKEZA KWA WINGI NOVEMBA 27, KUPIGA KURA

    November 15, 2024
  • MASHINE YA X-RAY MBIONI KUFIKA KITUO CHA AFYA TINDE

    November 15, 2024
  • Tazama zote

Video

wiki ya maji
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Muundo wa Taasisi
  • Muundo wa Taasisi
  • Video mbali mbali
  • Historia
  • Fomu ya Likizo
  • Leseni ya Makazi
  • Fomu ya Mkazi wa Ardhi kulipwa fidia

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • ofisi ya taifa ya takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Government Web Framework

Wasiliana nasi

    NIndo - Iselamagazi

    Anuani ya posta: 113 Shinyanga

    Simu: 0282-986382

    Simu: 0282-986382

    Baruapepe za watumishi: info@shinyangadc.go.tz/ded@shinyangadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.