• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Government Web Framework
Government Web Framework

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mwongozo wa Tovuti za Serikali

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Usafi na Manzingira
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na uhusiano
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki na Misitu
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Mipango
      • Kamati ya Masuala ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Elimu , Afya na Maji
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
    • Madiwani wa Kuchaguliwa
    • Madiwani wa Kuteuliwa
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Majarida
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Kanzi Data ya Picha
    • Hotuba
    • Habari
    • Video

RAS Shinyanga ataka mahusiano kazini Shinyanga DC yaboreshwe

Posted on: May 6th, 2021

Katibu Tawala Mkoa wa  Shinyanga Ndg. Albert Msovela leo tarehe 05.05.2021 ameitembelea Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga na Kuzungumza na Uongozi. Wakuu wa Idara na Wafanyakazi na kusisitiza sana kuhusu mahusiano baina ya mfanyakazi na Mfanyakazi na Idara na Idara.

Akizungumza kwenye Kikao cha Majumuisho, wakiwepo wakuu wa Idara, Mkurugenzi na Wafanya kazi wote, Katibu Tawala huyo alianza kwa kusisitiza  sana Upendo baina ya wafanya kazi na kuwataka wawe kitu kimoja. Alisema "Hata kauli mbiu ya Chama cha wafanyakazi inasema "Solidarity Forever"......ni wajibu na lazima wafanyakazi wa Shinyanga Dc Mpendane na kushirikiana. kuwe na "Coordination" kama ilivo mfumo wa mwili wa Binaadam.

Baadhi ya wakuu wa Idara na Wafanyakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Wakimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga.

Katibu Tawala huyo alisisitiza sana kwa wafanyakazi na Uongozi kuzingatia sana Sheria, kanuni, Maadili na Miongozo mbali mbali ya Utumishi wa Umma kwenye Utendaji wa Kazi zao na Maisha yao kwa ujumla.. alihimiza sana wafanyakazi waishi maisha yanayofanana na utumishi wa Umma. Aliwakumbusha Idara ya Utawala kuwa wao wana jukumu kubwa la kuhakikisha wafanyakazi wanazingatia sana sheria kanuni na taratibu za utumishi wa Umma. " nyie ndio Engine(Utawala) na Maafisa Rasilimali watu). zungumzeni na watu mjuwe shida zao, wakumbusheni wajibu na kuzingatia miongozo ya ufanyaji kazi serikalini mara kwa mara kabla ya kuwachukulia watu hatuwa za kinidhamu. ni vizuri tuelewane na kuwa wakali baada ya kuzungumza na kuridhika kuwa watu wamepewa nafasi ya kubadilika ila hawaoneshi dalili.

Katibu Tawala huyo alisisitiza sana Wafanyakazi kuwa na Siri za kiofisi na kutoku 'share' taarifa au document kwenye njia ambazo sio salama kama vile kutumia whatsapp ama email ambazo sio za Serikali. amewaambia wafanyakazi iwe marufuku uvujaji na usambazi wa kumbukumbu za kiofisi kwa watu wasihusika na shughuli za kiofisi.. aliwaonya wafanyakzi kuwa hatakuwa na simile kwa Mfanyakazi yeyote atevujisha taarifa na kumbukumbu za kiofisi kwani hilo ni miongoni mwa makosa makubwa ya kiutendaji.

Mheshimiwa Katibu Tawala huyo alisisitiza kwa kuzitaka Mamlaka kuwapatia mafunzo kazini wafanyakazi. "Tuwe na Mpango wa Mafunzo kwa wafanyakazi na kada zote na tuhakikishe kila mwaka kuna wafanyakazi wanaongezewa uwezo kwa kuhudhuria mafunzo ya kada zao". Alisisitiza kuona Mpango wa Mafunzo uliofanyiwa 'need Assesment' ya kutosha ili mafunzo hayo yawe na tija kwa wafanyakazi na Halmashauri kwa Ujumla.

Aliwaomya Wafanyakazi kutotegemea wanasiasa na kuacha taaluma zao na miongozo mbali mbali kwa kutaka urahisi kwenye maisha ya kazini hapa Shinyanga DC. "kuna watu wanapenda 'Vitonga, Senkeke'... Miteremko. wanaona wakijuhisisha na wanasiasa basi watakuwa salama kwenye mabaraza ya nidhamu. kawaonya wafanyakazi kuachana na mambo ya kupenda "Miteremko" bali wazingatie sheria, kanuni, maadili na miongozo ya utumishi wa Umma hapo watakuwa salama.

Ugeni wa Katibu tawala huyo uliwahiiza Idara ya utawala na rasilimali watu kuwa na mfumo wa ukusanyaji wa malalamiko ya wafanyakazi na kuyafanyia kazi ili kusiwe na migogoro maeneno ya kazi na kama ikiwepo isiwe ya kutishia maisha ya wafanyakazi na ufanyaji kazi. " Muwe na utaratiu wa wazi na utaozingatia faragha za watu, mpokee 'complains' na mzifanyie kazi hii itaisaidia sana kupunguza migogoro kazini,

kwa Upande wao wafanyakazi, walitaja kero zao na Kumuomba kuwa hiki alichokifanya leo basi kiwe endlevu. walimshukuru sana Katibu tawala kuja kuonana na kusikia kero za wafanyakazi. kitu ambacho kimeondowa woga walokuwa nao juu ya Kiongozi huyo na kwamba leo wamejisikia uhuru fulani kuzungumza nae na wamefarijika sana kushare "Issues zao" na kusikilizana walichokuwa nacho wafanya kazi kama kero. alichukuwa baadhi ya kero kwenda kuzifanyia kazi na zile ambazo aliziweza hapo hapo alizotolea Ufafanuzi.

Akizungumza kwenye kikao hiko, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Bi. Hoja N, Mahiba, (Picha chini)

alisisitiza Wafanyakazi kupendana na kuwa na "Team Work". kama alivotushauri Kiongozi wetu Katibu Tawala, Tupendane, Tushirikiane na kufanye kazi kama Mwili mmoja. alimshukuru sana Katibu tawala kuja na kuzungumza na wafanyakazi, alisema kafurahi sana kusikia wafanyakazi wameelewa sana Ujumbe ulioletwa na Kiongozi huyo toka Mkoani. Mkurugenzi alimkaribisha tena Katibu tawala huyo kila mara atapoona inafaa na anataka kuzungumza na wafanyakazi, Aliamuahidi kusimamia Maagizo yote aliyoyatowa kwenye kikao hiko na kuwa watajitahidi kuzingatia kanuni, sheria, madili na taratibu mbali mbali za utumishi wa umma kuhakikisha kero na maslahi ya Wafanyakazi wa Shinyanga DC yanatatuliwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 09, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA ( MCHUJO) KADA YA DEREVA DARAJA LA II April 15, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA TATU April 17, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI April 19, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MITI 1000 YAPANDWA KATA YA SALAWE KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 63 YA UHURU.

    December 09, 2024
  • BABA BORA, SAUTI YA UMMA NA WANAWAKE VIONGOZI WAPATIWA VITENDEA KAZI

    November 15, 2024
  • WANADIDIA WAOMBWA KUJITOKEZA KWA WINGI NOVEMBA 27, KUPIGA KURA

    November 15, 2024
  • MASHINE YA X-RAY MBIONI KUFIKA KITUO CHA AFYA TINDE

    November 15, 2024
  • Tazama zote

Video

wiki ya maji
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Muundo wa Taasisi
  • Muundo wa Taasisi
  • Video mbali mbali
  • Historia
  • Fomu ya Likizo
  • Leseni ya Makazi
  • Fomu ya Mkazi wa Ardhi kulipwa fidia

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • ofisi ya taifa ya takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Government Web Framework

Wasiliana nasi

    NIndo - Iselamagazi

    Anuani ya posta: 113 Shinyanga

    Simu: 0282-986382

    Simu: 0282-986382

    Baruapepe za watumishi: info@shinyangadc.go.tz/ded@shinyangadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.