• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Shinyanga District Council
Shinyanga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Usafi na Manzingira
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na uhusiano
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki na Misitu
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Mipango
      • Kamati ya Masuala ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Elimu , Afya na Maji
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
    • Madiwani wa Kuchaguliwa
    • Madiwani wa Kuteuliwa
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Majarida
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Kanzi Data ya Picha
    • Hotuba
    • Habari
    • Video

MKUU WA WILAYA MPYA MHE. SAMIZI ATEMBELEA SHINYANGA DC, AZUNGUMZA NA WATENDAJI WA KATA NA KUHUDHURIA BARAZA LAKE LA KWANZA LA MADIWANI KUPITISHA RASIMU YA BAJETI YA HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA

Posted on: February 2nd, 2023

Na. Dhulkifl H. Sungura - Kaimu Afisa Habari 



MKUU WA WILAYA YA SHINYANGA MHE. JOHARI SAMIZI LEO TAREHE 02 FEBRUARI 2023 AMEZUNGUMZA NA WATENDAJI WA KATA WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA. AKIZUNGUMZA NA WATENDAJI HAO KWENYE OFISI ZA HALMASHAURI HIYO, MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA ISELAMAGAZI.

  • Ataka kujuwa Miradi yote ya Maendeleo inayotekelezwa Shinyanga DC

“Mimi na Kamati ya Ulinzi na Usalama tunajipanga kuanza kukaguwa Miradi ya Maendeleo Shinyanga DC sasa kabla hatujaanza ZIara zetu, Watendai hakikisheni mnaweka taarifa zote sawa, za Miradi ya Maendeleo ili njia yetu wakati wa Ukaguzi iwe rahisi”. Lakini kingine alichosisitiza ni kuhakikisha Miradi yote ya Maendeleo kama ilivopangwa na kutekelezwa na Serikali ni lazima tuhakikishe inatimia na malengo yake kufikia. Tumepewa Dhamana na Mhe. Rais, hii ni heshima kubwa, lazima wote tuhakikishe hatumuangushi Mhe Rais wetu Mpendwa, hivyo Miradi ikamilike kwa kiwango ili hata Serikali ikija kuona miradi yake ijuwe kuwa kuna watu waliisimamia vyema.


  • Awataka sungungu kuwa wakali kwa jamii hasa watoto wasioenda shule kidato cha kwanza na shule za awali

Akizungumza kwenye Kikao kazi hicho, Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya akiwa ameambatana na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama (KU) ya Wilaya, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Dr. Nice R. Munissy na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Ngassa Mboje alisema kuwa ni lazima Jamii ijitahidi kuhakikisha inatafsiri MAONO ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassan kwa vitendo, hivo Wanafunzi wote wenye Sifa za kwenda Shule hawana budi kwenda Shule. “ Mh. Rais Kajenga Madarasa, Kaweka Madawati, anataka Watoto wote waende shule, sasa nasikia tuna Asilimia kama 11 na 10 kwa Msingi na Sekondari kuwa hawajaripoti shuleni,sitakubali nataka Asilimia 100 wote waende shule” Alisisitiza Mhe. Mkuu wa Wilaya. Asisitiza kuwa hata kama Mtoto hana sare za shule au Viatu, ni Agizo la Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kuwa waripoti shuleni hivo hivo,ili lengo litimie. Asisistiza Michenye itumike kweye Shughuli za Maendeleo pia na si kutumika tu mara watu wanapofumaniwa na wake za wat utu!!!

  • Ataka watu kutunza Mazingira na kuhakikisha utaratibu wa Kukata Miti hovyo unakoma Shinyanga DC

Akiongelea kuhusu Mazingira, Mheshimiwa DC Samizi alisema ameridhishwa alivokuwa njiani kutokea Manispaa ya Shinyanga alipoanza kuingia tu OLD SHINYANGA aliona kidogo kuna dalili za Uhai na kamwe sio kama huko alikotokea kwani kidogo kulikuwa na ukame sana. “ hapa nimeona dalili ya Uhai, hakuna misitu mingi, lakini kwa kweli kuna Dalili kabisa ya uhai, hili limenifurahisha. Kwani mimi nimuumini mkubwa wa Masuala ya Kutunza Mazingira, na ni lazima tuhimizane kuhakikisha Mazingira yetu yanakuwa safi na Salama na Miti haikatwi katwi hovyo”. Alisisitiza kuwa Mazingira usipoyatunza basi ujiandae na yenyewe kukuadhibu,ukiyadharau na yenyewe yatakudharau, sitaki kuona swala la mazingira Shinyanga DC yanadharauliwa.

  • Ahimiza Serikali za Vijiji kuwasomea Taarifa ya Mapato na Matumizi wananchi vijijini

Asisitiza ni kutekeleza takwa la kisheria kusoma mapato na matumizi kwa wananchi. Wanancho wana haki ya kujuwa mapato na matumizi ya Nguvu zao zote wanazojitolea kwenye Miradi ya Maendeleo na kamwe sio kuwaomba tu michango bila kuwapa taarifa za Mapato yao na matumizi yao. Asema Vijijini ni tatizo sana kusikia kwenye Mikutano mikuu ya vijiji Ajenda hiyo ikisomwa.

  • Awaomba Watendaji Ushirikiano wao Ulotukuka.

DC Samizi alisisitiza ili kuhakikisha Malengo ya Wilaya yanatimizwa, ni lazima wote tushirikiane, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na Watendaji wote, Bila ushirikiano wenu mimi Mkuu wa Wilaya nakuwa si lolote si chochote, nawaomba sana Tushirikiane kuhakikisha Gurudmu la Maendeleo kwenye Wilaya yetu linasonga mbele.

  • Ahudhuria Mkutano wa Baraza la Madiwani wa kupitia, Kujadili, na kupitisha Mpango wa Bajeti kwa mwaka 23/24

Akimaliza kikao kazi Hicho, Mhe, Mkuu wa Wilaya aliongozana na Mwenyekiti wa Halmashauri na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwenda Kwenye Baraza la Madiwani kupitia, kujadili na kupitisha Rasimu ya Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka 23/24.

Aliwapongeza Halmashauri kwa Bajeti nzuri na Waheshimiwa Madiwani jinsi walivoijadili na kuhimiza Vipaumbele vyote vilivoibuliwa na Waheshimiwa Madiwani havina budi kutekelezwa kwenye Bajeti ya mwaka 23/24. "Bajeti ni nzuri, mjipange kuhakikisha Vyanzo vyote vya Mapato mlivovikasimia mnavikusanya na kuwa Mtatumia kadiri mlivojipangia".



Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI - AJIRA ZA MUDA USIMAMIZI WA MIRADI November 04, 2022
  • TANGAZO LA KAZI - AJIRA ZA MUDA USIMAMIZI WA MIRADI November 04, 2022
  • UPANGISHAJI WA MAJENGO YA OFISI NA NYUMBA ZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA ZILIZOPO MANISPAA YA SHINYANGA July 02, 2020
  • TANGAZO MAPOKEZI YA FEDHA February 09, 2021
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA KAMATI YA WATU WENYE ULEMAVU

    February 28, 2023
  • MKUU WA WILAYA MPYA MHE. SAMIZI ATEMBELEA SHINYANGA DC, AZUNGUMZA NA WATENDAJI WA KATA NA KUHUDHURIA BARAZA LAKE LA KWANZA LA MADIWANI KUPITISHA RASIMU YA BAJETI YA HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA

    February 02, 2023
  • BARAZA LA WAFANYAKAZI SHINYANGA DC LAPITISHA RASMI YA MPANGO NA BAJETI YA HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA KWA MWAKA 2023/24

    January 31, 2023
  • BARAZA LA WAFANYAKAZI SHINYANGA DC LAPITISHA RASMI YA MPANGO NA BAJETI YA HALAMSHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA KWA MWAKA 2023/24

    January 31, 2023
  • Tazama zote

Video

wiki ya maji
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Muundo wa Taasisi
  • Video mbali mbali
  • Historia
  • Fomu ya Likizo
  • Leseni ya Makazi
  • Fomu ya Mkazi wa Ardhi kulipwa fidia

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • ofisi ya taifa ya takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    NIndo - Iselamagazi

    Anuani ya posta: 113 Shinyanga

    Simu: 0282-986382

    Simu: 0282-986382

    Baruapepe za watumishi: info@shinyangadc.go.tz/ded@shinyangadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa