• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Government Web Framework
Government Web Framework

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mwongozo wa Tovuti za Serikali

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Usafi na Manzingira
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na uhusiano
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki na Misitu
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Mipango
      • Kamati ya Masuala ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Elimu , Afya na Maji
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
    • Madiwani wa Kuchaguliwa
    • Madiwani wa Kuteuliwa
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Majarida
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Kanzi Data ya Picha
    • Hotuba
    • Habari
    • Video

MKUTANO WA WADAU WA MRADI WA UBORESHAJI WA USALAMA WA MILKI ZA ARDHI WILAYA YA SHINYANGA

Posted on: June 29th, 2024

Na Monica Mnanka, Shinyanga DC


 Katibu Tawala wa Wilaya ya Shinyanga Bw. Saidi Kitiga akimwakilisha Mkuu wa Wilaya hiyo ametoa wito kwa 

wote wakataoshiriki moja kwa moja katika utekelezaji wa mradi wa uboreshaji wa usalama wa milki za ardhi 

unaotarajiwa kuanza Julai mosi 2024 kufanya kazi kwa uaminifu na uadilifu wa hali ya juu kwa kuzingatia uzalendo. 


“ Niwasihi kila mmoja wetu kwa nafasi yake atimize wajibu wake kikamilifu ili kuleta matokeo chanya......., tuunganishe

 nguvu zetu kwa pamoja kuwezesha maeneo yetu ya vijiji 15 kupangwa, kupimwa na kusimamiwa vyema kwa ustawi

 wa Taifa letu.” Alisisitiza Bw.Kitiga


Hayo ameyasema Juni 28,2024 wakati akifungua mkutano wa wadau kujadili utekelezaji wa mradi huo uliofanyika

 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga uliopo Iselamagazi. Katika mkutano huo pia

 amewataka watekelezaji wa mradi kutekeleza majukumu yako kwa weledi, haki na usawa ili kuepusha migogoro

 kwa wananchi.


Akizungumza wakati wa mkutano huo, Bw. Kitiga amesema mradi huo umelenga kuboresha usalama wa milki za 

ardhi kwa kupanga , kupima na kusajili milki ardhi ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga inakusudiwa 

kutoa Hati Milki 62,000 katika maeneo ya vijiji 15 vya kata 9 . Vijiji hivyo ni pamoja na kijiji cha Samuye, Isela, 

Singita, Jomu, Nyambui, Didia, Mwanono, Solwa, manheigana, Songambele, Mwakitolyo, Nyaligongo, Iselamagazi, 

Mwamakaranga na mwongozo.


Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Bw. Edward Maduhu akitoa neno la ufunguzi

 amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano waTanzania, Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan mradi ambao 

unakwenda kutatua na kuondoa kero mbalimbali za ardhi ikiwemo kuwapatia hati milki na kuondoa migogoro

 ya mipaka.


Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ni miongoni mwa zaidi ya halmashauri 60 zinazotarajiwa kunufaika na mradi huo.
















Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 09, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA ( MCHUJO) KADA YA DEREVA DARAJA LA II April 15, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA TATU April 17, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI April 19, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MITI 1000 YAPANDWA KATA YA SALAWE KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 63 YA UHURU.

    December 09, 2024
  • BABA BORA, SAUTI YA UMMA NA WANAWAKE VIONGOZI WAPATIWA VITENDEA KAZI

    November 15, 2024
  • WANADIDIA WAOMBWA KUJITOKEZA KWA WINGI NOVEMBA 27, KUPIGA KURA

    November 15, 2024
  • MASHINE YA X-RAY MBIONI KUFIKA KITUO CHA AFYA TINDE

    November 15, 2024
  • Tazama zote

Video

wiki ya maji
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Muundo wa Taasisi
  • Muundo wa Taasisi
  • Video mbali mbali
  • Historia
  • Fomu ya Likizo
  • Leseni ya Makazi
  • Fomu ya Mkazi wa Ardhi kulipwa fidia

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • ofisi ya taifa ya takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Government Web Framework

Wasiliana nasi

    NIndo - Iselamagazi

    Anuani ya posta: 113 Shinyanga

    Simu: 0282-986382

    Simu: 0282-986382

    Baruapepe za watumishi: info@shinyangadc.go.tz/ded@shinyangadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.