• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Government Web Framework
Government Web Framework

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mwongozo wa Tovuti za Serikali

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Usafi na Manzingira
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na uhusiano
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki na Misitu
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Mipango
      • Kamati ya Masuala ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Elimu , Afya na Maji
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
    • Madiwani wa Kuchaguliwa
    • Madiwani wa Kuteuliwa
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Majarida
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Kanzi Data ya Picha
    • Hotuba
    • Habari
    • Video

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA AWASHUKURU WADAU NA KUWAOMBA KUENDELEA NA JITIHADA ZA KUPAZA SAUTI ZA KUTOKOMEZA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO

Posted on: October 23rd, 2024

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Dkt. Kalekwa Kasanga amewaomba Wadau wanoatekeleza afua za Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) kuendelea kupaza sauti  na kutoa elimu ya kutokemeza ukatili ili kunusuru kundi hilo.

Ameyasema hayo akiwa anahairisha kikao cha kamati ya ulinzi wa Wanawake na Watoto ngazi Halmashauri  leo Oktoba 23, 2024 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ambapo kipeekee ameishukuru taasisi ya Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake Tanzania (WFT-TRUST) kwa kuiwezesha Halmashauri takribani miaka 6 kutekeleza shughuli mbalimbali za kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

“Sambamba na hatua zinazoendelea za kubadili umri wa Watoto wa kike kuolewa bado kama wadau endeleeni kupambania hali ya ulinzi na usalama wa Mwanamke na Mtoto” Dkt. Kasanga ameongeza.

Kwa upande wake Mratibu wa MTAKUWWA Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Bi. Aisha Omari amesema kupitia utekelezaji wa mpango huo kwa mwaka huu  wameweza kuwaokoa Wanafunzi 7 wa kike katika ndoa za utotoni na wawili kati yao kuwarejesha shule za Sekondari za bweni za Salawe  na Isaka.

Aidha, Bi. Aisha ameongeza kuwa mbali na mafanikio mengi wamefanikiwa pia kufanya uratibu na uundwaji wa madawati na mabaraza  ya watoto nje na ndani ya shule na kufanikiwa kupata madawati 144 ya shule ya Msingi na 32 ya Sekondari. Mabaraza 20 ya Kata pamoja na Mabaraza 99 ya Vijiji yanayoendelea na kazi za kuelimisha maswala ya ukatili nje na ndani ya shule.


Akitoa neno la shukrani kwaniaba ya Wadau wengine Meneja Miradi kutoka shirika la Thubutu Africa Initiative (TAI) Bi. Pascalia Mbuguni amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji kwa kupokea changamoto na mapendekezo yao, pamoja na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano wa kutoa elimu kwa jamii ili waweze kuachana na mila na desturi kandamizi zinazopelekea kufanya ukatili dhidi Wanawake na Watoto.


Awali wakati wa ufunguzi wa kikao hicho Ndg. David Rwazo kwa niaba ya Mkurugenzi  Mtendaji aliwakumbusha Wadau mbali na kupigania kundi la wanawake na watoto vile vile wasisahau kuwaelemisha wanaume umuhimu wa elimu jumuishi katika malezi ya familia.

 Mpango  kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto ni mpango kazi wa Taifa wa miaka mitano mpango ambao ulipelekea Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na Wadau kuandaa mkakati  wa Mkoa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto kwa kuangalia changamoto za Mkoa na kuziwekea mikakati ya utekelezaji.

Mkakati huu katika  Halmashauri ya Wiliya ya Shinyanga umetekelezwa na mashirika yasiyo ya kiserikali  YAWE, RAFIKI SDO, POLISI DAWATI LA JINSIA NA WATOTO WILAYA YA SHINYANGA ,YWL, GCI, SPC, WEADO, RADIO FARAJA NA Halmashauri ya Shinyanga yenyewe kwa awamu mbalimbali kupitia fedha ya ruzuku kutoka (WFT-TRUST).

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 09, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA ( MCHUJO) KADA YA DEREVA DARAJA LA II April 15, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA TATU April 17, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI April 19, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MITI 1000 YAPANDWA KATA YA SALAWE KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 63 YA UHURU.

    December 09, 2024
  • BABA BORA, SAUTI YA UMMA NA WANAWAKE VIONGOZI WAPATIWA VITENDEA KAZI

    November 15, 2024
  • WANADIDIA WAOMBWA KUJITOKEZA KWA WINGI NOVEMBA 27, KUPIGA KURA

    November 15, 2024
  • MASHINE YA X-RAY MBIONI KUFIKA KITUO CHA AFYA TINDE

    November 15, 2024
  • Tazama zote

Video

wiki ya maji
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Muundo wa Taasisi
  • Muundo wa Taasisi
  • Video mbali mbali
  • Historia
  • Fomu ya Likizo
  • Leseni ya Makazi
  • Fomu ya Mkazi wa Ardhi kulipwa fidia

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • ofisi ya taifa ya takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Government Web Framework

Wasiliana nasi

    NIndo - Iselamagazi

    Anuani ya posta: 113 Shinyanga

    Simu: 0282-986382

    Simu: 0282-986382

    Baruapepe za watumishi: info@shinyangadc.go.tz/ded@shinyangadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.