• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Government Web Framework
Government Web Framework

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mwongozo wa Tovuti za Serikali

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Usafi na Manzingira
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na uhusiano
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki na Misitu
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Mipango
      • Kamati ya Masuala ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Elimu , Afya na Maji
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
    • Madiwani wa Kuchaguliwa
    • Madiwani wa Kuteuliwa
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Majarida
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Kanzi Data ya Picha
    • Hotuba
    • Habari
    • Video

Mbunge Jimbo la Solwa kuwatibia Majeruhi walioko Hospitali, Machimboni Nyandolwa.

Posted on: September 16th, 2021

Mbunge wa Jimbo la Solwa Mhe. Ahmed Salum Ally leo tarehe 16.09.2021 akiwa kwenye Ziara ya Madiwani kukaguwa shughuli za uchimbaji Madini na Mapato ya Serikali na Halmashauri katika Machimbo kwenye Kitongoji cha Nyandolwa, Kata ya Mwenge, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ameahidi kuwatibia Majeruhi wote walioko Hospitali mpaka watoke baada ya Sehemu ya Machimbo ya Mgodi huo kuanguka na Baadhi ya watu kujeruhiwa.

Akiongea Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Ngassa Mboje, baada ya kutambulishwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Bi. Nice R Munissy, aliwaambia wachimbaji hao kuwa haya ni mpenzi ya Mwenyezi Mungu Mtukufu na kuwa Baraza limeona lije liwape pole kutokana na yalotokea siku ya jana tarehe 15/09/2021 katika maeneo ya Machimbo baada ya baadhi ya Mashmo kuporomoka.

Alisistiza kuwa Baraza limeona lije liwaone ikiwa ni sehemu ya kazi yake ya kutatuwa changamoto za wananchi. " Halmashauri ni kiungo kati ya Wananchi na Serikali kuu, tumekuja kupata changamoto zenu na kwenda kuzifanyia kazi. kama zitatushinda basi tutaziwasilisha Serikali kuu" alisisitiza Mwenyekiti huyo wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Akizungumza Mwenyekiti wa Chama Wilaya ya Shinyanga, Mwenyekiti Alitowa kwanza pole na kusema wenyewe kama Chama cha Mapinduzi wameguswa sana na tukio hili, na kuwa walivosikia Mhe. Mbunge na waheshimiwa Madiwani wanakuja kuwapa pole basi wakaona nao wajiunge nao. " Tunatowa pole sana kwa Jamii ya Wachimbaji Nyandolwa".  aliwaomba Wachimbaji kuchukuwa tahadhari zote zinazohitajika wakati wa Kuchimba na kutafuta Madini lakini akawatia moyo sana wananchi hao kuwa hiyo kazi haiwez kuachwa. "Mnafanya kazi nzuri sana na mnatupatia mapato,sio rahisi muache hii kazi bali ni muhimu tu kuchukuwa tahadhari zote zinazohitajika".

Akizungumza Mhe. Mbunge wa Jimbo la Solwa alianza kutowa salam za pole kwa kuwaambia wananchi hao kuwa baada ya kupata taarifa hii, aliamuwa kusitisha shughuli zake na kuja kuwapa pole wananchi. alisema tukio hili limeleta huzuni lakini tuko pamoja. alisema waliulizia kuwa kuna watu bado wanapata matibabu, akasema kwa hawa wanaopata matibabu yeye yuko tayari kuwahudumia mpaka wapate nafuu. aliwaahidi wachimbaji hao kuwa kwa kushirikiana na kamishna wa Madini mkoa wa Shinyanga, watahakikisha Eneo la Machimo la Nyandolwa linakuwa salama. swala la Usalama wenu ntalipeleka Wizarani, lazima muwe salama, mchape kazi kwa raha zenu.

Jambo la pili ni kama mnavoona, kuna uongozi wote kuanzia Mkurugenzi, Mwenyekiti wa Chama na wa Halmashauri, Madiwani wa Wataalam wote tumekuja hapa kuwapa pole. tunaendelea kufatilia tukio hili na usalama wenu, tutaendelea kufatilia mpaka pale tutapoona kuwa mnafanya kazi salama na kuwa  mazingira yanaboreshwa ili mfanye kazi kwa Amani na utulivu. Mheshimiwa Mbunge alisema leo si siku ya kuongea mengi kwani bado watu tuna majonzi. kwa hayo machache alishukuru sana kupata fursa ya kuongea na wachimbaji na wafanyakazi wa migodini.

Akihitimisha Mazungumzo hayo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Bi Nice alisema kwanza anawapongeza sana wachimbaji na wafanyakazi wa Mgodi kwa utulivu waliouonyesha kipindi cha matatizo ya kuporomoka kwa baadhi  ya Mashimo ya Migodi, pili alimshukuru Mhe. Mbunge kwa kuamuwa kuwasaidia Majeruhi wote wa Mgodi na kuwashughulikia afya zao mpaka watakapopona kabisa. 

Aliwashukuru sana Wachimbaji kwa kuwa tangu walivoachana jana jioni mpaka leo hajasikia vurugu zozote na watu wanaendelea kuchapa kazi kwenye maeneo ambayo ni salama. ila alitumia nafasi hiyo kwashukuru sana wananchi kwa weledi wao wa kuchaguwa Viongozi wasikivu. "mmeona shida imetokea jana tu lakini leo Viongozi  wote wako tayari hapa nanyi. hii inaonyesha kwamba nyie ni wananchi makini ndio maana mkachaguwa Viongozi wasikivu na wenye Huruma."

Alihitimisha kwa kuwambia kuwa kwa Amani walioionyesha atawapa ushirikiano wote unaohitajika kama Mkurugenzi mwenye dhamana ya Halmashauri hii na kuwa atahakikisha changamoto zote zilizo ndani ya uwezo wetu kama Halmashauri zitatatuliwa kwa haraka na zile zilizo nje ya uwezo wetu tutashirikiana sana na Viongozi wa juu tuhakikishe zinatatuliwa kwa wakati. kwa kuwa bado kuna wasiwasi kuwa kuna wenzetu bado wako kwenye mashimo basi tuache mazungumzo haya ili kazi ya kuwatafuta wenzetu na masalia iendleee, aliwaoma wananchi hao kuwa Mungu awabariki sana na anawatakia kila la kheri kwenye shughuli zao.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 09, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA ( MCHUJO) KADA YA DEREVA DARAJA LA II April 15, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA TATU April 17, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI April 19, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MITI 1000 YAPANDWA KATA YA SALAWE KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 63 YA UHURU.

    December 09, 2024
  • BABA BORA, SAUTI YA UMMA NA WANAWAKE VIONGOZI WAPATIWA VITENDEA KAZI

    November 15, 2024
  • WANADIDIA WAOMBWA KUJITOKEZA KWA WINGI NOVEMBA 27, KUPIGA KURA

    November 15, 2024
  • MASHINE YA X-RAY MBIONI KUFIKA KITUO CHA AFYA TINDE

    November 15, 2024
  • Tazama zote

Video

wiki ya maji
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Muundo wa Taasisi
  • Muundo wa Taasisi
  • Video mbali mbali
  • Historia
  • Fomu ya Likizo
  • Leseni ya Makazi
  • Fomu ya Mkazi wa Ardhi kulipwa fidia

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • ofisi ya taifa ya takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Government Web Framework

Wasiliana nasi

    NIndo - Iselamagazi

    Anuani ya posta: 113 Shinyanga

    Simu: 0282-986382

    Simu: 0282-986382

    Baruapepe za watumishi: info@shinyangadc.go.tz/ded@shinyangadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.