• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Government Web Framework
Government Web Framework

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mwongozo wa Tovuti za Serikali

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Usafi na Manzingira
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na uhusiano
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki na Misitu
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Mipango
      • Kamati ya Masuala ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Elimu , Afya na Maji
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
    • Madiwani wa Kuchaguliwa
    • Madiwani wa Kuteuliwa
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Majarida
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Kanzi Data ya Picha
    • Hotuba
    • Habari
    • Video

MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA WAISHUKURU SERIKALI KWA KUENDELEA KUTOA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: March 7th, 2024

Mkutano wa Baraza la Madiwani wa robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2023/2024 umefanyika Machi 7, 2024 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa lengo la kupokea taarifa za utekelezaji wa kazi katika kipindi cha robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2023/2024 kutoka Kamati za Kudumu. Kamati hizo ni Kamati ya Fedha Uongozi na Mipanga, Kamati ya Afya, Elimu na Maji, Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira, Kamati ya Maadili na Kamati ya Kudhibiti Ukimwi.


Akizungumza wakati wa kufungua Baraza hilo, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe.Nicodemus L.Simon ambaye ni Diwani wa Kata ya Masengwa ametoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutenga fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri hiyo.


Aidha, akiwasilisha taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri, Dkt Nuru Yunge amesema Halmashauri imepokea fedha kiasi cha Sh. 541,800,000.00 kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya ujenzi wa miradi mbalimbali katika sekta ya Elimu, Afya, Maji na huduma nyingine za Jamii kwa kipindi cha robo ya pili.


“Natoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Halmashauri fedha hizi kwa kuwa zitasaidia kwa sehemu kubwa kupunguza uhaba wa miundombinu ya elimu,” alishukuru Dkt. Yunge.


Akiwakilisha taarifa ya Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango kwa niaba ya Mwenyekiti wa kamati hiyo, Diwani wa Kata ya Didia Mhe. Luhende P Masele alieleza kuwa katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2023/2024, kamati imetembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa na ameipongeza Serikali kwa uwekezaji mkubwa inayoifanya katika halmashauri hiyo.



Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga

 Mhe. Nidodemus L. Simon akiongoza Mkutano wa Baraza la Madiwani 

kujadili taarifa za Kamati za Kudumu katika mkutano wa Baraza la 

Madiwani katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2023/2024. 


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Dkt. Nuru Yunge akiwakilisha taarifa ya

 Mkurugenzi Mtendaji wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani


Mhe. Luhende Masale, Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi ya

 maendeleo katika kipindi cha robo ya pili kwa mwaka wa fedha 

2023/2024 kutoka  Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango kwa niaba ya

 Mwenyekiti wa Kamati.


Mwenyekiti wa Kamati ya Afya, Elimu na Maji Mhe. Isack Sengelema, 

ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Iselamagazi akiwasilisha taarifa ya 

utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika kipindi cha robo ya Pili kwa

 mwaka wa fedha 2023/2024  kutoka  Kamati hiyo.


Mwenyekiti wa Kamati Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira 

Mhe. Sonya J. Mhela, ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Itwangi 

akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika 

kipindi cha robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2023/2024.


Mjumbe wa Kamati ya Kudhibiti Ukimwi, Mhe. Susana N. Malembela

 ambaye ni Diwani Viti Maalum akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa

 miradi ya maendeleo katika kipindi cha robo ya pili kwa mwaka wa 

fedha 2023/2024 kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 09, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA ( MCHUJO) KADA YA DEREVA DARAJA LA II April 15, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA TATU April 17, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI April 19, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MITI 1000 YAPANDWA KATA YA SALAWE KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 63 YA UHURU.

    December 09, 2024
  • BABA BORA, SAUTI YA UMMA NA WANAWAKE VIONGOZI WAPATIWA VITENDEA KAZI

    November 15, 2024
  • WANADIDIA WAOMBWA KUJITOKEZA KWA WINGI NOVEMBA 27, KUPIGA KURA

    November 15, 2024
  • MASHINE YA X-RAY MBIONI KUFIKA KITUO CHA AFYA TINDE

    November 15, 2024
  • Tazama zote

Video

wiki ya maji
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Muundo wa Taasisi
  • Muundo wa Taasisi
  • Video mbali mbali
  • Historia
  • Fomu ya Likizo
  • Leseni ya Makazi
  • Fomu ya Mkazi wa Ardhi kulipwa fidia

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • ofisi ya taifa ya takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Government Web Framework

Wasiliana nasi

    NIndo - Iselamagazi

    Anuani ya posta: 113 Shinyanga

    Simu: 0282-986382

    Simu: 0282-986382

    Baruapepe za watumishi: info@shinyangadc.go.tz/ded@shinyangadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.