Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Shinyanga Bi.Azza Hamad Hilal amewataka wanawake mkoani hapa kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi za uongozi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu, pamoja na uchaguzi mkuu ujao.
Azza ameeleza hayo Machi 8, 2019 kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika kiwilaya kwenye kata ya Lyabukande halmashauri ya wilaya ya Shinyanga huku mashirika mbalimbali yanayojishughulisha na shughuli mbalimbali za maendeleo zikiwemo kupinga ukatili dhidi ya wanawake pia yalishiriki.
Alisema wanawake wana uwezo mkubwa wa kuongoza jamii , na kutolea mfano Mama Samia Suluhu Hassan namna anavyochapa kazi katika kuwatumikia watanzania katika kutatua matatizo yao hivyo aliwataka wajitokeze kwa wingi kwenye uchaguzi wa mwaka huu wa Serikali za Mitaa kunia kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.
"Halmashauri hii ya wilaya ya Shinyanga ina jumla ya vijiji 126 ,lakini viongozi wanawake ambao ji wenyeviti wapo wawili tu, hii ni aibu hivyo nawasihi wanawake wenzangu tujitokeze kwa wingi kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwenye uchaguzi wa mwaka huu na hata uchaguzi mkuu ujao mwakani ,"amesema Azza.
Pia aliwataka wanaume kuwaunga mkono wanawake kwa kuwapigia kura hasa pale wanapomuona anafaa kuwa kiongozi bora , na kuondoa dhana ya mfume dume kwa kuwaona ni viumbe dhaifu na hatimaye kuacha kuwachagua.
Naye mwenyekiti wa halmashauri hiyo ya wilaya ya Shinyanga Ngassa Mboje , aliwataka wanaume kuacha tabia ya kunyanyasa wanawake , huku akiahidi halmashauri itaendele kutatua changamoto mbalmbali zinazowakabili wanawake ikiwemo na utoaji wa fedha za mikopo kwa wingi.
Kwa upande wa risala ya wanawake wilayani ikisomwa na Lucy Fabian , ilitaja baadhi ya changamoto ambazo wanakabiliana nazo ,kuwa ni ukosefu wa fedha za mikopo ya kutosha ,kubakwa pamoja na kubaguliwa kwenye nafasi za za kuwania uongozi .
Aidha kauli mbiu ya mwaka huu ya maadhimisho ya siku ya wanawake duniani inasema"Badili fikra ili kufikia usawa wa kijinsia kwa maendeleo endelevu"
NIndo - Iselamagazi
Anuani ya posta: 113 Shinyanga
Simu: 0282-986382
Simu: 0282-986382
Baruapepe za watumishi: info@shinyangadc.go.tz/ded@shinyangadc.go.tz
Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.