• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Government Web Framework
Government Web Framework

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mwongozo wa Tovuti za Serikali

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Usafi na Manzingira
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na uhusiano
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki na Misitu
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Mipango
      • Kamati ya Masuala ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Elimu , Afya na Maji
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
    • Madiwani wa Kuchaguliwa
    • Madiwani wa Kuteuliwa
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Majarida
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Kanzi Data ya Picha
    • Hotuba
    • Habari
    • Video

KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YAMPONGEZA MKURUGENZI HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA KWA USIMAMIZI MZURI WA UJENZI WA JENGO LA UTAWALA

Posted on: April 18th, 2024

Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Ngassa Mboje leo Aprili 18, 2023 imefanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo robo ya tatu kwa mwaka 2023/2024 yenye thamani ya jumla ya Tsh. 511,986,829.46. Miradi iliyotembelewa ni pamoja na ujenzi wa jengo la utawala la Halmashauri, ujenzi wa bweni la watoto wenye mahitaji maalum, ujenzi wa matundu ya vyoo 26 vya wanafunzi katika Shule ya Msingi ya Isela na kutembelea kikundi cha vijana cha Usanda Kwetu.

Akizungumza wakati wa kutembelea mradi wa Jengo la Utawala la halmashauri uliopo katika kijiji cha Mwamakaranga kata ya Iselemagazi, Mhe, Mboje amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Ndg. Kisena Mabuba kwa usimamizi mzuri wa ukamilishaji wa jengo la utawala ambalo limefikia hatua nzuri ya utekelezaji wa mradi huo.


“…kubwa ninaloliona ni pongezi kubwa kwako Mkurugenzi na team yako……, kwa sababu tumeona mabadiliko ya kasi na viwango, spidi tunaiona sasa baada ya wewe kuchukua hatua.


 Naye Ndg. Mabuba wakati akiishukuru Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango kwa kutembelea mradi huo, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuridhia halmashauri kupata fedha kwa ajili ya mradi huo.  Ndg Mabuba aimeitaarifu kamati hiyo kuwa kwa mwaka ujao wa fedha 2024/2025, halmashauri imeidhinishiwa kiasi cha Shilingi Bilioni moja kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo la utawala.


Kasi ya ujenzi wa jengo la utawala ni juhudi mahususi ambazo zimechukuliwa ili kuharakisha ukamilishaji wa jengo hilo ambalo linatarajiwa kuanza kutumika mapema Mei mwaka huu.


“saa nyingine Mhe. Tunakuja hapa tunakuwa wakali kweli kweli, lengo ni kuhakikisha kuwa tunafikia malengo ambayo tumejiwekea, mimi nina imani kabisa kabla ya mwisho wa mwaka wa fedha huu, Shinyanga DC tutakuwa nyumbani kwetu, tukiishi kwetu na sio sehemu nyingine na wananchi wetu tutawahudumia kutokea hapa, kuhamia mimi Mhe. Mwenyekiti nasubiri milango tu” alisisitiza Mabuba.


Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa sasa zipo katika jengo la muda lililopo eneo la Iselamagazi lililoanza kutumika Novemba mwaka 2019 baada ya kuhama kutoka katika Ofisi zake za Makao Makuu ya halmashauri zilizokuwa zilizokuwa Manispaa ya Shinyanga. Kuhama   kulilenga halmashauri kuhamia katika eneo lake la utawala ili kurahisisha huduma kwa wananchi.


Muonekano wa nje wa hatua ya ujenzi wa jengo la Utawala la Halmashauri

 ya Wilaya ya Shinyanga


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Shinyanga, Mhe. Ngassa Mboje 

(mwenye tshirt ya blue) akipokea maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji

 wa Halmashauri kuhusu hatua za ujenzi wa jengo  la utawala la

 Halmashauri hiyo.


Wajumbe wa Kamati wakikagua mradi wa jengo la utawala


Picha ya pamoja ya wajumbe wa kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango na

 wataalamu halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 09, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA ( MCHUJO) KADA YA DEREVA DARAJA LA II April 15, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA TATU April 17, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI April 19, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MITI 1000 YAPANDWA KATA YA SALAWE KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 63 YA UHURU.

    December 09, 2024
  • BABA BORA, SAUTI YA UMMA NA WANAWAKE VIONGOZI WAPATIWA VITENDEA KAZI

    November 15, 2024
  • WANADIDIA WAOMBWA KUJITOKEZA KWA WINGI NOVEMBA 27, KUPIGA KURA

    November 15, 2024
  • MASHINE YA X-RAY MBIONI KUFIKA KITUO CHA AFYA TINDE

    November 15, 2024
  • Tazama zote

Video

wiki ya maji
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Muundo wa Taasisi
  • Muundo wa Taasisi
  • Video mbali mbali
  • Historia
  • Fomu ya Likizo
  • Leseni ya Makazi
  • Fomu ya Mkazi wa Ardhi kulipwa fidia

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • ofisi ya taifa ya takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Government Web Framework

Wasiliana nasi

    NIndo - Iselamagazi

    Anuani ya posta: 113 Shinyanga

    Simu: 0282-986382

    Simu: 0282-986382

    Baruapepe za watumishi: info@shinyangadc.go.tz/ded@shinyangadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.