• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Government Web Framework
Government Web Framework

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mwongozo wa Tovuti za Serikali

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Usafi na Manzingira
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na uhusiano
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki na Misitu
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Mipango
      • Kamati ya Masuala ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Elimu , Afya na Maji
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
    • Madiwani wa Kuchaguliwa
    • Madiwani wa Kuteuliwa
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Majarida
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Kanzi Data ya Picha
    • Hotuba
    • Habari
    • Video

Ziara ya Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Wilayani Shinyanga

Posted on: November 9th, 2019

Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Professa Joyce Ndalichako  leo Novemba 9,2019 amefanya ziara kwenye   halmashauri ya wilaya ya Shinyanga ambapo pamoja na mengine amezindua na kuweka Jiwe la msingi kwenye Majengo ya uthibiti ubora wa Shule.


Kwenye halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, ameweka jiwe la Msingi katika Jengo la Uthibiti ubora katika kata ya Iselamagazi pamoja na kulizindua ambapo limeshakamilika kwa asilimia kubwa.

Akizungumza mara baada ya kukagua jengo hilo na kuweka mawe ya Msingi na kuzindua ,Prof. Ndalichako amewataka wathibiti ubora wa shule kufanya kazi kwa bidii ili kuinua taaluma hapa nchini.

Amesema wathibiti ubora ndiyo kioo cha taaluma hapa nchini, hivyo wanapaswa kuzikagua shule ipasavyo, ili ziweze kutoa elimu bora kwa wanafunzi na kuzalisha taifa la wasomi.

"Serikali ya awamu ya Tano inatumia pesa nyingi sana kwenye sekta ya elimu ili kuhakikisha taifa linakuwa na watu wasomi, hivyo nawaagiza wathibiti ubora wa shule msimamie taaluma ipasavyo," amesema  Prof. Ndalichako.

Katika hatua nyingine ameonya kitendo cha wanafunzi kuonyeshwa mitihani ya kuhitimu shule, na kubainisha kuwa yule atakayekamatwa kufanya hivyo atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Naye Katibu Tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela ,amesema serikali kupitia wizara ya elimu imetoa kiasi cha zaidi ya Shilingi Milioni 600 kujenga Majengo ya Uthibiti ubora katika halmashauri Nne za mkoa wa Shinyanga.

Ametaja halmashauri hizo kuwa ni Kahama Mji, Ushetu, Manispaa ya Shinyanga na halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, ambapo kila Jengo limegharimu Shilingi Milioni 152.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack , amesema kipaumbele cha mkoa huo ni elimu, ambapo watahakikisha kiwango cha ufaulu kinakuwa juu pamoja na wanafunzi kupata elimu bora na siyo bora elimu.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Tecknolojia Profesa Joyce Ndalichako, akikagua Ujenzi wa Jengo la Uthibiti ubora wa Shule lililopo Kata ya Iselamagazi halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

Mthibiti ubora wa Shule halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Joyce Andrew akisoma taarifa ya ujenzi wa Jengo la Uthibiti ubora wa Shule lililopo Kata ya Iselamagazi halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 09, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA ( MCHUJO) KADA YA DEREVA DARAJA LA II April 15, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA TATU April 17, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI April 19, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MITI 1000 YAPANDWA KATA YA SALAWE KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 63 YA UHURU.

    December 09, 2024
  • BABA BORA, SAUTI YA UMMA NA WANAWAKE VIONGOZI WAPATIWA VITENDEA KAZI

    November 15, 2024
  • WANADIDIA WAOMBWA KUJITOKEZA KWA WINGI NOVEMBA 27, KUPIGA KURA

    November 15, 2024
  • MASHINE YA X-RAY MBIONI KUFIKA KITUO CHA AFYA TINDE

    November 15, 2024
  • Tazama zote

Video

wiki ya maji
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Muundo wa Taasisi
  • Muundo wa Taasisi
  • Video mbali mbali
  • Historia
  • Fomu ya Likizo
  • Leseni ya Makazi
  • Fomu ya Mkazi wa Ardhi kulipwa fidia

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • ofisi ya taifa ya takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Government Web Framework

Wasiliana nasi

    NIndo - Iselamagazi

    Anuani ya posta: 113 Shinyanga

    Simu: 0282-986382

    Simu: 0282-986382

    Baruapepe za watumishi: info@shinyangadc.go.tz/ded@shinyangadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.