• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Government Web Framework
Government Web Framework

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mwongozo wa Tovuti za Serikali

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Usafi na Manzingira
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Teknolojia, Habari, Mawasiliano na uhusiano
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki na Misitu
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha na Mipango
      • Kamati ya Masuala ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Elimu , Afya na Maji
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
    • Madiwani wa Kuchaguliwa
    • Madiwani wa Kuteuliwa
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu
    • Majarida
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Kanzi Data ya Picha
    • Hotuba
    • Habari
    • Video

WAKULIMA, MSICHANGANYE PAMBA NA MAZAO MENGINE KWENYE SHAMBA MOJA - RC MACHA

Posted on: November 9th, 2024

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewakumbusha wakulima wa zao la pamba kuacha tabia ya kuchanganya na mazao mengine kwenye shamba moja huku akisisitiza pia juu ya umuhimu mkubwa wa kung'olea maotea kwani tupo nyuma ya wakati.


RC Macha ameyasema haya leo tarehe 9 Novemba, 2024 katika mkutano wa hadhara uliolenga kuwakumbusha wakulima wa pamba katika Kitongoji cha Mwabusiga wilayani Kishapu wakulima ambao pia wamepata elimu na ushauri wa namna bora ya kulima eneo dogo kwa tija zaidi na Balozi wa Pamba nchini ndugu Aggrey Mwanri.

"Ndugu zangu wakulima wa zao la pamba hapa Mwabusiga, niwaombe sana na kuwakumbusha kwa dhati kabisa kuacha tabia ya kuchanganya zao la pamba na mazao mengine katika shamba moja, kwa kufanya hivyo hatutaona mafanikio tarajiwa kutoka kwenye kilimo hiki na hakutakuwa na maana yoyote tena ya kulima pamba," amesema RC Macha.


Awali akitoa hamasa ya kilimo cha pamba Mwanri amesema kuwa tumekuwa tukifanya makosa makubwa sana kuchelewa kung'olea maotea na kuondoa masalia katika zao la pamba kwakuwa madhara yake ni makubwa sana ambapo amesema kwa mujibu wa utaratibu wa kilimo bora masalia na maotea hupaswa kuondolewa kabla ya tarehe 15 / 9 / 2024 na ukichelewa kufanya hivyo unazalisha pamba mapepe na isiyokuwa na ubora.

"Niwaombe sana ndugu zangu Wanabusiga tuendelea kufuata ushauri na maelekezo ya wataalam wetu wa kilimo na wengine ili tuweze kuwa na kilimo bora cha kisasa ambapo utapaswa kulima eneo dogo na lenye kukuletea tija zaidi na tusichanganye mazao katika shamba moja na tung'olee maotea na kuondoa masalia kabla ya kuanza kilimo cha msimu unaofuata," amesema Mwanri.


Aidha ndg. Buluma Kalidusi ambaye ni Mkaguzi wa Pamba Kanda ya Magharibi amewataka wakulima kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za kilimo cha pamba ambapo ndani yake zinawakataza kabisa wakulima kutekeleza kilimo cha pamba kwa ujanjaujanja ikiwa ni pamoja na kuondoa masalia na maotea katika shamba kabla ya msimu mwingine wa kilimo yaani Septemba 15 ya kila mwaka (Sheria Na. 2 ya mwaka 2001 na kanuni zake)

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 09, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA ( MCHUJO) KADA YA DEREVA DARAJA LA II April 15, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA TATU April 17, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI April 19, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MITI 1000 YAPANDWA KATA YA SALAWE KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 63 YA UHURU.

    December 09, 2024
  • BABA BORA, SAUTI YA UMMA NA WANAWAKE VIONGOZI WAPATIWA VITENDEA KAZI

    November 15, 2024
  • WANADIDIA WAOMBWA KUJITOKEZA KWA WINGI NOVEMBA 27, KUPIGA KURA

    November 15, 2024
  • MASHINE YA X-RAY MBIONI KUFIKA KITUO CHA AFYA TINDE

    November 15, 2024
  • Tazama zote

Video

wiki ya maji
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Muundo wa Taasisi
  • Muundo wa Taasisi
  • Video mbali mbali
  • Historia
  • Fomu ya Likizo
  • Leseni ya Makazi
  • Fomu ya Mkazi wa Ardhi kulipwa fidia

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • ofisi ya taifa ya takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Government Web Framework

Wasiliana nasi

    NIndo - Iselamagazi

    Anuani ya posta: 113 Shinyanga

    Simu: 0282-986382

    Simu: 0282-986382

    Baruapepe za watumishi: info@shinyangadc.go.tz/ded@shinyangadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.